Wakati wa vikao vya awali vya habari Dar es salaam na Mwanza.
Katika wiki ya 20 na 24 ya mwezi wa nne TMF ilifanya jumla ya vikao vitatu vya awali vya habari Dar es salaam na waandishi wa habari waliopatiwa ruzuku mara ya kwanza ya maombi. Mazungumzo hayo ya awali yalifanyika pia mkoani Mwanza tarehe sita mwezi wa tano.vikao vilifanywa na washauri wenye uzoefu waliochaguliwa na TMF kuwapatia ruzuku waandishi wa habari washindi.vikao vilijumuisha majadiliano kimakundi kuhusu vigezo vya uandishi bora wa habari na waandishi wa habari walikuwa na vikao vya mmoja mmoja na washauri wao ambapo waliweza kujadili maada walizozipendekeza wao wenyewe. kusudi la vikao hivi vya awali ilikuwa ni kuwapa nafasi waandishi wa habari kushiriki katika mijadala ili wapate vidokezo vitavyowasaidia namna ya uboreshaji wa habari zao .Waandishi wa habari sasa wanategemewa kwenda mahali pa kazi na kuanza kufanya kazi zao.Waliopewa ruzuku watakuwa na nafasi ya kuwa na washauri wao wakati watapohitaji msaada au ushauri wakati wa kazi.Mara waandishi wa habari watapochapisha au kurusha hadithi zao watarudi TMF kuakisi au kwa ajili ya vikao vya awali. Tumepokea miitiko mingi chanya kutoka kwa washiriki na tunatazamia kuwafuatilia waliopewa ruzuku katika safari zao.
